Soma Wasifu wa Walioteuliwa

Soma Wasifu wa Walioteuliwa

Piga kura sasa

Sasa, ni wakati wa kupigia kura waleta mabadiliko wenye asili ya Kiafrika unaoamini wanapaswa kutunukiwa kama washindi wa tuzo za Mwanaharakati wa Mwaka, Vuguvugu la Mwaka, pamoja na Mwanaharakati Bora wa Kisanaa wa Mwaka!

Piga kura sasa

Mnamo mwaka wa 2019, Africans Rising ilianzisha tuzo za Uanaharakati za Africans Rising ili kuwatambua wanaharakati wa kijamii wa Kiafrika wanaofanya kazi kwa ajili ya haki, amani na utu kwa Waafrika. Mpango wa tuzo hiyo umepata usaidizi maarufu hivi kwamba umeendelea kupanuka. Mnamo 2020, Tuzo za uanaharakati za Africans Rising zilitambua uanaharakati wa kibinafsi na vile vile wa pamoja, na mwaka wa 2021 Tuzo za Uanaharakati zilipanuka na kuwa jukwaa la kuonyesha vipaji vya ubunifu vya wasanii wa Afrika.

Mpango wa Tuzo za uanaharakati za Africans Rising wa mwaka wa 2022 utatambua uanaharakati wa Kiafrika kupitia utoaji wa tuzo tatu: tuzo ya Africans Rising ya mwanaharakati bora wa mwaka, tuzo ya Africans Rising ya harakati bora ya mwaka, na tuzo ya Africans Rising ya mwanaharakati bora wa kisanaa.

Mpango wa utoaji tuzo utafanywa katika awamu tatu: wito wa umma kwa ajili ya uteuzi, mchakato wa kuhakikiwa na kamati iliyoteuliwa ili kuchagua wateule bora zaidi katika kila kitengo, na kipindi cha upigaji kura kwa umma mtandaoni, na duru ya upigaji kura mtandaoni, iliyo wazi kwa wanachama wa Africans Rising pekee, ili kubaini washindi, na vile vile washindi wa nafasi ya pili ya kila tuzo. Wateule wote watatu bora zaidi wataalikwa kuhudhuria hafla ya tuzo itakayoandaliwa mtandaoni.

Tuzo za uanaharakati za Africans Rising zinanuia kutambulisha na kuendeleza wanaharakati, pamoja na harakati za Kiafrika, na vile vile kuangazia ushirikishi wao wa uanaharakati kama njia ya kufanikisha mabadiliko chanya katika jamii za Kiafrika. Kupitia mfano wa wateule na washindi wa tuzo, mpango huu wa tuzo unaonyesha uanaharakati kama swala la kudhaminiwa katika jamii ya Kiafrika, na unalenga kuhamasisha vitendo sawa miongoni mwa wahusika wengine katika asasi za kiraia katika bara la Afrika pamoja na ughaibuni.

Mpango wa tuzo za uanaharakati za Africans Rising unaunga mkono na kuleta pamoja wanaharakati na harakati katika mtandao wa kimataifa wa Waafrika wanaojihusisha na vitendo visivyo vya ukatili ili kukuza haki, amani, na utu kwa Waafrika wote popote walipo.

WASHINDI WA ZAMANI

Katika awamu ya kwanza ya mpango huu wa tuzo za Africans Rising, Jean-Marie Kalonji, mwanaharakati kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo alichaguliwa kuwa mshindi wa tuzo la mwanaharakati wa Africans Rising wa Mwaka wa 2019.

Mnamo mwaka wa 2020, kati ya washindani 20 walioteuliwa katika kategoria mbili, Asha Jaffar Harun, mwanaharakati na mwanahabari nchini Kenya, alichaguliwa kuwa Mwanaharakati wa Mwaka, na Tournon La Page, harakati ya kimataifa ya kuunga mkono demokrasia, ikapigiwa kura kuwa harakati ya mwaka. Tuzo hizo zilitolewa katika kikao chao Utawala Bora katika Afrika Magharibi, iliyoandaliwa nchini Benin.

Washindi wafuatao walipigiwa kura na wanachama wa Africans Rising katika mpango wa Tuzo za Uanaharakati wa 2021: Mwanaharakati wa Mwaka, Wilson Atumeyi (Nigeria), Vuguvugu la Mwaka, la Vijana kwa Bunge (Zambia), Mwanaharakati Bora wa Kisanaa, Joice Zau (Angola). Tuzo zilitolewa ana kwa ana na vile vile kupitia mtandaoni katika sherehe maalum mjini Abuja, Nigeria.

UTEUZI

Uteuzi wa tuzo hizo hufanywa na raia kupitia tovuti ya Africans Rising (africansrising.org). ). Baada ya uteuzi, wateule watahakikiwa na jopo teule la majaji, kisha wagombeaji wachache wataorodheshwa kama wateuliwa bora zaidi. Kwa kila kategoria (Mwanaharakati Bora wa Mwaka, Harakati Bora ya Mwaka na Mwanaharakati Bora wa Kisanaa wa Mwaka), wateule wawili bora zaidi watachaguliwa kuwakilisha Afrika Kaskazini, Afrika Mashariki, Afrika ya Kati, Afrika Magharibi, Kusini mwa Afrika, na wanadiaspora, kwa jumla ya wateule 36.

Watakaorodheshwa kama wateule bora zaidi wataarifiwa kwa barua pepe au WhatsApp. Wateule hao wataombwa kuwasilisha picha, wasifu, na video (kwa hiari) ili kuonyesha kazi zao. Habari hizo zitawekwa kwenye tovuti ya Africans Rising ili wanachama wetu wapate kujifunza zaidi kuhusu wateule, pamoja na uharakati zao wanapoamua ni nani wa kumpigia kura kama chaguo lao kuu wakati wa duru ya mwisho ya upigaji kura.

DURU YA MWISHO YA UPIGAJI KURA

Baada ya wateule bora zaidi, katika kitengo cha mwisho kutangazwa, kutakuwa na kipindi cha mwisho cha upigaji kura ambapo ni wanachama wa Africans Rising waliojiandikisha kupitia hifadhidata yetumpya ya uanachama pekee ndio watakaoweza kupigia kura mtandaoni wale wagombea wanaowafikiri kuwa wanapaswa kupokea Tuzo ya uharakati ya Africans Rising. Ikiwa bado haujakuwa mwanachama wa Africans Rising, basi unaweza kuwa mojawapo ya wanachama, kwa kujaza fomu yetu ya usajili wa uanachama. Ikiwa wewe ni mwanachama wa Africans Rising aliyesajiliwa kabla ya tarehe 31 Oktoba 2022, basi ni lazima ujisajili upya kupitia hifadhidata yetu mpya ya uanachama.. Upigaji kura utafanywa kupitia hifadhidata ya wanachama wa Africans Rising na kila mpiga kura anaweza kupiga kura moja kwa chaguo lake kuu katika kila kitengo.

Washindi wataamuliwa kwa idadi ya kura watakazozipata. Mteuliwa aliye na idadi kubwa zaidi ya kura, akiwemo mshindi wa kwanza, atapokea taji la mwaka (Mwanaharakati bora wa Mwaka wa 2021, Harakati bora ya Mwaka wa 2021 au Mwanaharakati bora wa Kisanaa wa Mwaka wa 2021). Wateule wanaopokea nambari ya pili na ya tatu kwa wingi wa kura, watatajwa mshindi wa pili na wa pili, mtawalia, katika kategoria yao. Kisha, washindi wote watatu katika kila kitengo wataalikwa kuhudhuria hafla ya tuzo, itakayoandaliwa mtandaoni.

SHEREHE ZA TUZO

Matokeo ya kura yatafichuliwa na wapokeaji tuzo watatangazwa wakati wa hafla ya tuzo, itakayoandaliwa mtandaoni. Wateule watatu wataopokea jumla ya kura za juu zaidi katika kila kitengo wataalikwa kwenye hafla ya tuzo za uanaharakati, itakayoandaliwa mtandaoni. Hii itakuwa fursa kwao kupokea tuzo zao na kuonyesha uharakati zao kupitia jukwaa la kimataifa la Africans Rising. Washindi wa Nafasi ya Kwanza, Washindi wa Nafasi ya Pili, na Washindi wa Nafasi ya Tatu vile vile watatangazwa wakati wa hafla hiyo.

SHEREHE ZA TUZO

Matokeo ya kura yatafichuliwa na wapokeaji tuzo watatangazwa wakati wa hafla ya tuzo, itakayoandaliwa mtandaoni. Wateule watatu wataopokea jumla ya kura za juu zaidi katika kila kitengo wataalikwa kwenye hafla ya tuzo za uanaharakati, itakayoandaliwa mtandaoni. Hii itakuwa fursa kwao kupokea tuzo zao na kuonyesha uharakati zao kupitia jukwaa la kimataifa la Africans Rising. Washindi wa Nafasi ya Kwanza, Washindi wa Nafasi ya Pili, na Washindi wa Nafasi ya Tatu vile vile watatangazwa wakati wa hafla hiyo.

VIGEZO VYA UTEUZI

MWANAHARAKATI BORA WA MWAKA

Tuzo ya Africans Rising ya mwanaharakati bora wa mwaka(Africans Rising Activist of the Year Award) ni tuzo ya kila mwaka ya kumtambua mtu binafsi (mwanaharakati) kwa kazi yake katika swala la haki ya kijamii, kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya Waafrika walioko barani Afrika, pamoja na/au walioko ughaibuni.

Kufuzu kama mteule wa Tuzo ya Africans Rising ya Mwanaharakati Bora wa Mwaka, Mteule lazima atimize vigezo vifuatavyo:

  1. Mteule lazima awe Mwafrika
  2. Mteule lazima awe mwanachama wa Africans Rising*
  3. Mteule lazima awe na umri wa miaka 35 au chini
  4. Uanaharakati wa mteule lazima uonyeshe ueledi wao kuhusu maswala ya haki ya kijamii
  5. Mteule lazima awe anajihusisha na kazi isiyo na ukatili
  6. Mteule lazima awe na uwezo wa kutoa ushahidi wa kazi yao katika maswala ya haki ya kijamii, kwa muda usiopungua miaka miwili

HARAKATI BORA YA MWAKA

Tuzo la Africans Rising ya Harakati Bora ya Mwaka(Africans Rising Movement of the Year Award) ni tuzo ya kila mwaka ya kutambua harakati, jumuiya au shirika kwa kazi zao katika swala la haki ya kijamii kuleta mabadiliko chanya katika maisha ya Waafrika walioko barani Afrika, pamoja na/au walioko ughaibuni.

Kufuzu kama mteule wa Tuzo ya Africans Rising ya Harakati Bora ya Mwaka(Africans Rising Movement of the Year Award), Mteule lazima atimize vigezo vifuatavyo:

  1. Shirika lazima liwe limeanzishwa na kuongozwa na Waafrika au vizazi vya Waafrika
  2. Shirika lazima liwe mwanachama wa Africans Rising*
  3. Shirika lazima liwe linashiriki katika maswala ya kijamii
  4. Mafanikio ya shirika lazima yaonyeshe kazi yake katika maswala ya haki ya kijamii
  5. Shirika lazima liwe linajihusisha na kazi isiyo na ukatili
  6. Shirika lazima liwe na uwezo wa kutoa ushahidi wa kazi yao katika maswala ya haki ya kijamii, kwa muda usiopungua miaka miwili

MWANAHARAKATI BORA WA KISANAA WA MWAKA

Tuzo hii ya Africans Rising, ya Mwanaharakati Bora wa Kisanaa (Africans Rising Artistic Activist of the Year Award) ni tuzo mpya. Tuzo hii ya Africans Rising, ya Mwanaharakati Bora wa Kisanaa wa Mwaka ni tuzo inayowatambua wasanii barani Afrika pamoja na/au katika diaspora (ughaibuni), wanaotumia sanaa zao kuendeleza mabadiliko chanya ya kijamii katika maisha ya Waafrika.

itawatambua wasanii wanaotumia sauti zao kuendeleza mabadiliko chanya ya kijamii katika maisha ya Waafrika walioko barani Afrika, Mteule lazima atimize vigezo vifuatavyo:

  1. Mteule lazima awe Mwafrika
  2. Ikiwa kazi imeonyeshwa katika lugha nyingine isipokuwa Kiingereza au Kifaransa, basi mteule lazima atoe tafsiri ya kazi hiyo katika lugha ya Kiingereza au Kifaransa.
  3. Mteule lazima awe mwanachama wa Africans Rising*
  4. Mteule lazima awe na umri wa kati ya miaka 18 – 35 au chini
  5. Kazi ya ubunifu ya mteule lazima ihusiane na masuala ya haki ya kijamii
  6. Mteule lazima awe anajihusisha na kazi isiyo na ukatili
  7. Mteule lazima awe na uwezo wa kutoa ushahidi wa kazi yao katika maswala ya haki ya kijamii kwa muda usiopungua miaka miwili

Jiandikishe kama mwanachama wa Africans Rising ili kupiga kura

A votação para Premiação de Activismo do Africans Rising 2022 terá início no dia 28 de Novembro às 6:00 GMT e terminará aos 11 de Dezembro às 11:59 GMT.

Unaweza kujiandikisha hapa

RATIBA YA TUZO

  • Okt 31 – Nov 13 -Wito wa Uteuzi
  • Nov 14 – Nov 20 – Mapitio ya Jopo ili Kuwateua wateule bora zaidi
  • Nov 21 – 27 – Kuwasiliana na wateule; Kupokea picha za mteule, video, wasifu; Kuandaa jukwaa la kupiga kura
  • Nov 28 – Des 11 – Kipindi cha Mwisho cha Kupiga Kura
  • Wiki ya Desemba 12 – Tuzo za uanaharakati za Africans Rising – Sherehe ya Tuzo itakayoandaliwa Mtandaoni(Tarehe itaamuliwa karibuni)

TUZO

The winners of the 2022 Africans Rising Activist of the Year Award will be presented with the following awards:

  1. Pesa ya Tuzo ya $1000 (Mshindi), $500 (Mshindi wa Kwanza), $300 (Mshindi wa Pili)
  2. Vibao vya Tuzo
  3. Kushiriki katika programu za Africans Rising
  4. Zawadi za kumbukumbu kutoka kwa Africans Rising

The winners of the 2022 Africans Rising Movement of the Year Award will be presented with:

  1. Pesa ya Tuzo ya $1000 (Mshindi), $500 (Mshindi wa Kwanza), $300 (Mshindi wa Pili)
  2. Vibao vya Tuzo
  3. Mafunzo ya kipekee yaliyoandaliwa na Africans Rising, kuhusu ujenzi wa harakati, uongozi, au kampeni za mabadiliko ya kijamii
  4. Mwakilishi mwanachama ataalikwa kuhudhuria mafunzo au kongamano ya Africans Rising
  5. Zawadi za kumbukumbu kutoka kwa Africans Rising

The winners of the 2022 Africans Rising Artistic Activist of the Year Award will be presented with:

  1. Pesa ya Tuzo ya $1000 (Mshindi), $500 (Mshindi wa Kwanza), $300 (Mshindi wa Pili)
  2. Vibao vya Tuzo
  3. Kushiriki katika programu za Africans Rising
  4. Zawadi za kumbukumbu kutoka kwa Africans Rising

Wateule na washindi wote wa Tuzo za uanaharakati watapata fursa ya kushirikiana kwa kujitolea, na Africans Rising, kuandaa uhamasishaji kuhusu masuala muhimu katika kazi zao, na uanachama wetu.